Thursday, October 8, 2015

Edward Lowassa Akiwa Arusha.




Mgombea wa uraisi kwa tiketi ya CHADEMA Edward Lowassa amewataka wananchi wa Ngaramtoni Arusha wamchague ili aweze kumaliza kero zao mapema mara baada ya kuingia Ikulu.

“Nipeni madaraka tarehe 25 niwaonyeshe kazi” alisema Lowassa.
Edward Lowasa ameendelea kufanya kampeni za lala salama huku akisisitiza vipaumbele vya serikali yake mara atakapo pata idhini ya wananchi kuongoza nchi.
“Nitashughurikia tatizo la Elimu na Afya nchini kwani elimu ni chanzo cha mafanikio ya mambo mengine”.alisema Lowassa.
Hata hivyo wananchi katika mkutano katika uwanja wa Mringa walipaza sauti wakimwambia kwa sauti “Maji” “Umeme” naye  akasisitiza wampe madaraka tarehe 25 ili awashughulikie wale ambao hawawajibiki kutatua matatizo ya wananchi.
Ameendelea kuwaahidi walimu na wakulima kuwa maisha yao yatabadilika kwa kuboresha mazingira ya utendaji kazi wao na kuahidi serikali kutokuwa chanzo cha migogoro na matatizo.

No comments:

Post a Comment

google +

google +
chris kyando

FIND US ON FACEBOOK