Wednesday, October 9, 2013

Baada Ya Kulewa,Dawa Ya “Hang'over” Hii Hapa…




kwa kawaida watu wengi wanaotumia pombe wanaelewa sana ninapozungumzia ‘hang'over’.kwa ambao hawatambui  hii ni ile hali ya mtu kujisikia mchovu,kichwa kuuma na hali nyingine nyingi za kukera mara baada ya kuamka  iwapo usiku wa jana uliutumia kwa kunywa pombe hasa kwa kiwango kikubwa.

kutokana na hali hiyo watu wengi wamekuwa wakitumia njia mbalimbali ili kurudisha hali yao kuwa ya kawaida,wengine hutumia supu na maji kwa wingi,wengine huamini kunywa tena pombe wakiamini dawa ya moto ni moto na nyinginezo.
watafiti  wa china wamegundua katika utafiti wao kwamba soda aina ya sprite inaweza kuwa ni chaguo bora zaidi kutibu tatizo la “hangover”.wao waliangalia chanzo cha mtu kupata matatizo mara baada ya kulewa pombe.wakafuatilia mchakato mzima jinsi mwili unavyofanya kazi kwa mtu akinywa pombe,wakagundua kwamba kimeng’enya kiitwacho kitaalamu Alcohol Dehydrogenase(ADH) hubadili kimea cha pombe kuwa “Acetaldehyde” ambayo inaaminika kuwa ndiyo chanzo cha matatizo yatokanayo na kunywa pombe ambayo hudumu kwa muda mrefu pamoja na “hang'over”. Pia kimeng’enya kiitwacho kitaalamu Aldehyde Dehydrogenase(ALDH)  hugeuza Acetaldehyde kuwa Acetate ambayo inaaminika kuwa in chanzo cha faida zitokanazo na kunywa pombe.
katika utafiti wao walitumia vinywaji tofauti  57 vikijumuisha chai na vinywaji  vilivyotengenezwa kwa kuchanganywa na  madini ya kaboneti ambapo soda ya sprite ni mojawapo.katika vinywaji hivyo walilinganisha jinsi ADH  na ALDH  zinavyofanya kazi.wakaona kwamba kila kinywaji kina madhara tofauti kikiwa kwenye ADH na ALDH huku vinywaji vingi vikionekana kuchochea ADH kufanya kazi ambayo hupelekea matokeo mabaya baada ya kunya pombe huku vikikandamiza utendaji kazi wa ALDH,lakini sprite(inayojulikana kwa jina la Xue bi huko China) ilionekana kuongeza utendaji kazi wa ALDH  huku ikikandamiza utendaji kazi wa ADH na hivyo  kupunguza madhara yatokanayo na kunywa pombe.
kwa maoni yangu,kwa wale ambao wamekuwa wakisumbuliwa na hali hiyo ni vyema wakajaribu kutumia utafiti huu pengine unaweza kuwarudisha katika ubora wao katika utendaji wa kazi hasa ukizingatia watu wengi hasa wanaotumia pombe siku ya jumapili hujikuta wakishindwa kufanya kazi zao kiufanisi siku ya jumatatu.pia kama unadhani kuna njia nyingine bora waweza kuacha ujumbe wako hapo chini.Sishauri mtu yeyote kunywa pombe,lakini ukiwa mtumiaji, huu ni ushauri wangu.

No comments:

Post a Comment

google +

google +
chris kyando

FIND US ON FACEBOOK